Posts

Showing posts with the label HABARI

KIBITI Mambo Shwari: Gesti na Viwanja Vyapanda Bei

Image
                Maisha ya Kibiti sasa ni shwari hamna shari na tayari bei za vitu kama viwanja na huduma kama za nyumba za kulala wageni (gesti) zimeanza kupanda bei upya kama ilivyokuwa awali. Taarifa hiyo yenye kuashiria dalili njema za kurejea kwa amani na utulivu kwa wakazi wa wilaya hiyo iliyopo mkoani Pwani, ilithibitishwa na jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wake, Barnabas Mwakalukwa. Hivi karibuni, wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji mkoani Pwani, zilielekea kuwa tishio jipya la ulinzi na usalama nchini baada ya kuwapo kwa taarifa za mauaji ya kila mara ya watu wasio na hatia, wakiwamo viongozi wa vijiji, vitongoji, polisi na hata raia wa kawaida. Jumla ya watu zaidi ya 30 waliripotiwa kuuawa katika matukio tofauti ya kipindi cha takribani mwaka mmoja tu uliopita. Tishio hilo la usalama Kibiti lilisababisha baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo kukimbia na kwenda kuishi maeneo mengine nchini na pia, taarifa zilisambaa hata kwenye mitandao mba...

WATU 200 Wakamatwa Kwa Tuhuma za Dawa za Kulevya, Unyang’anyi

Image
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar ES salaam limeendelea kufanya misako na operesheni kali ambapo kuanzia 10/7/2017 mpaka tarde 16/7/2017 limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 200 kwa makosa mbalimbali ya uhalifu.

Sheria Mpya za Madini Mfupa mgumu kwa wawekezaji

Image
                     Wakati Serikali ikiendelea kutafuta njia za kudhibiti kikamilifu rasilimali za nchi baada ya kupitisha sheria mpya ya maboresho ya Sheria ya Madini iliyopendekeza mambo kadhaa, wawekezaji katika sekta hiyo wameanza kutishika na kuanza kujiondoa. Baada ya kupitishwa kwa sheria hiyo, tayari mwekezaji mmoja kutoka Australia, Ian Middlemas kupitia kampuni yake ya Cradle Resources, amekosa dili la dola 55 milioni za Marekani (Sh121 bilioni) kupitia mradi wa uchimbaji wa madini ya niobium Panda Hill, uliopo nchini. Kufuatia hatua hiyo, wataalamu kadhaa wa masuala ya uchumi wamesema ni lazima sheria hizo zitakuwa zimewashtua wawekezaji. Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Utafiti wa Kupunguza Umaskini (Repoa), Dk Abel Kinyondo alisema watakimbia kwa muda mfupi tu. Profesa Haji Semboja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema kutaibuka baadhi ya kampuni ambazo zitafanya hivyo ili kutishia Serikali ili ichanganyikiwe na kub...

MAITI yaokotwa Bwawani

Image
Mwili wa mtu ambaye hajafahamika umeokotwa katika bwawa la maji lililopo Mtaa wa Nkende Shuleni katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. Hili ni tukio la tatu la watu kuuawa kisha miili yao kutupwa kwenye mabwawa ya maji katika kipindi cha miezi sita iliyopita. Hivi karibuni, mwili wa kijana ambaye alikuwa dereva wa bodaboda ulikutwa ukiwa umetupwa katika eneo hilo hilo. Kamanda wa Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe, amethibitisha kuokotwa kwa mwili huo na kubainisha kuwa Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi ili kuwabaini watu wanafanya mauaji hayo. Chareles Kisege, ambaye ni mwenyekiti wa mtaa wa Nkende Shuleni na James Nyangai mwenyekiti wa mtaa wa Kimusi, wamesema matukio hayo yamezusha hofu miongoni mwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo. Wamitaka serikali kuchukua hatua za haraka kuwadhibiti wauaji hao. Licha juhudi za wananchi kutaka kuuopoa mwili huo, zoezi hilo limekuwa zito na gumu kutokana na kukosa zana. Hata hivyo, mwenyekiti wa chama cha waendesha bodaboda wilayani...

Matamshi ya Magufuli kuhusu wasichana wa shule waliotungwa mimba yawakasirisha wanawake Tanzania

Image
Rais wa Tanzania John Magufuli ameshutumiwa kwa matamshi yake kwamba wasichana wanaojifungua hawafai kuruhusiwa kurudi shule. Ombi la mitandao ya kijamii limewekwa huku shirika moja la wanawake barani Afrika likitoa hamasa ya kumtaka rais Magufuli kuomba msamaha kwa matamshi hayo. Bwana Magufuli aliwaonya wasichana wa shule katika mkutano wa hadhara siku ya Jumatatu kwamba ''unaposhika mimba mambo yako yamekwisha''. Sheria iliopitishwa mwaka 2002 inaruhusu kutimuliwa kwa wasichana waliotungwa mimba wakiwa shuleni. Sheria hiyo inasema kuwa wasichana wanaweza kufukuzwa shuleni kwa ''makosa yanayokiuka maadili na ndoa''. Makundi ya haki ya wanawake yamekuwa yakiishinikiza serikali kubadilisha sheria hiyo. Magufuli ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara katika mji wa Chalinze ,takriban kilomita 100 magharibi mwa mji wa Dar es Salaam alisema kuwa kina mama hao wachanga hawatasoma vyema iwapo wataruhusiwa kurudi shule. Baada ya kupiga hesabu ,ata...

INASIKITISHA:Mwanafunzi wa Miaka 13 Abakwa Korongoni Hadi Kufa

Image
Mwanafunzi  wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 13 anayesoma Shule ya Msingi Kipanga wilayani Tanganyika mkoa wa Katavi, amebakwa hadi kufa na watu wasiojulikana, ambao waliutupa mwili wake korongoni. Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Benedict Mapujila alisema kitendo hicho cha kikatili ni cha juzi ya saa 11:30 kijijini humo . Alisema siku ya tukio hilo, mwanafunzi huyo wa kike aliondoka nyumbani kwao kama kawaida yake kwenda shule. Hata hivyo, hakurudi tena kwao na kusababisha wasiwasi mkubwa kwa wazazi wake, kwa kuwa hakuwa na tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani. Wazazi wake walikuwa na wasiwasi mkubwa kwa binti yao kuchelewa kurudi nyumbani, hivyo waliamua kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji chao. Viongozi hao wa kijiji na wananchi, walianza kumsaka binti huyo kwenye maeneo mbalimbali bila kukata tamaa. “Ilipofika saa kumi na moja na nusu ya jioni waliukuta mwili wa mwanafunzi huyo ukiwa umetupwa korongoni na kubaini kuwa alikuwa amebakwa huku sehemu zake za siri ziki...

Lowassa, Sumaye, Mabata Watema Cheche Msibani

Image
Viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani wamelaani kitendo cha serikali ya mkoa wa Kilimanjaro cha kuzuia uwanja wa Mashujaa kutumika kwa ajili ya ibada ya kuaga mwili wa marehemu Philemon Ndesamburo, na kudai kuwa kililenga kuendeleza chuki ya kisiasa.  Katika hatua nyingine, wameshangazwa na CCM kutokuwa na muwakilishi katika ibada ya kuuga mwili wa Ndesamburo aliyefariki dunia wiki iliyopita wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya KCMC Moshi. Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa alisema kitendo hicho kimelenga kudhibiti demokrasia. “Nawapongeza kwa maandalizi haya. ila kwa hili inaonyesha jitihada za kudhibiti demokrasia zinaendelea, watu hawa ni wa kuwasamehe bure." Naye mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Pwani, Fredrick Sumaye alisema “Hata njia za kupitisha maiti nazo zinalindwa hizi chuki tukiacha zijengwe hatutakua hai, wananchi hatutaweza kuwaonea muda mrefu. Ila mbegu  ya amani aliyoipanda Ndesamburo itaendelea kuzaa aliyoyasimamia.”  Wakati akitoa salam...

Baada ya Kutumbuliwa..Prof Muhongo ..Mbunge wa Upinzani Ajitokeza Kumteta..!!!

Image
                                          Mjadala wa mchanga wa dhahabu (makinikia) umeibuka tena bungeni mbunge akiwatuhumu wenzake, huku akimtetea Profesa Sospeter Muhongo kuwa ametolewa madarakani kama vile mbuzi wa kafara. Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea  amesema Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa wawajibike kwa kuwa ni wahusika wa mikataba mibovu ya madini. Amesema makinikia yana dhahabu lakini yanayofanyika yanaweza kuliingiza Taifa kwenye mgogoro wa kidiplomasia, kisheria na wa kimahakama. Kubenea ametoa shutuma hizo jana (Ijumaa) akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/18. Amesema Rais John Magufuli amwajibishe pia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani. Mbunge huyo amesema hapuuzi nia njema ya Rais Magufuli ya kuwatumik...

Rais Magufuli awaonya wakwepa kodi

Image
  Rais wa Tanzania John Magufuli amesema kuanzishwa kwa mfumo mpya wa serikali wa ukusanyaji kodi kwa njia ya Kielekroniki, (Data Center) itakuwa dawa kwa wale wote wanaokwepa kulipa kodi. Akizindua uanzishwaji wa mfumo huo, jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema ili kuondoa malalamiko ya wale wanaodai kubambikiziwa kodi isiyo sawa na wale wanaokwepa kulipa kodi, ufumbuzi ni kuwepo kwa kituo hicho. Amesisitiza kuwa ni lazima kila mmoja alipe kodi, ili kuweza kupata mapato yatakayoweza kutumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya nchi. Aidha ameyataka makampuni mbalimbali yaliyoko nchini, yakiwemo ya simu, na Wizara zote kuingia katika mfumo huo mpya wa serikali wa ukusanyaji kodi kwa njia ya kielekroniki, ambao ni muhimu wa ustawi na maendeleo ya nchi.   Rais Magufuli pia amesema kuanzisha kwa mfumo huo ni ukombozi wa kupunguza kero za muungano. ''...Kwa sababu ukijaza vocha yako huko Zanzibar hiyo pesa itaenza Zanzibar, ukinunulia vocha yako Kigoma au Moshi hiyo...

Sakata la Mchanga Lahamia Zanzibar..Wawakilishi Waikaba Koo SMZ..!!!

Image
Msimamo wa baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi juu ya kuizuia Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifungo na Uvuvi ya mwaka 2017-2018 hadi pale watakapopata majibu yenye kueleweka juu ya hatua ya rasilimali ya mchanga kuhodhiwa na Serikali badala ya wananchi wenyewe kama ilivyokuwa awali utapata majibu leo wakati waziri wake, Hamad Rashid atakapojibu hoja zao. Hatua ya wajumbe hao imetokana na malalamiko ya wananchi waliokuwa wakimiliki mashamba ambayo sasa yanachimbwa mchanga chini ya uangalizi wa Serikali huku wao wakiambulia patupu. Awali, mashamba hayo yalikuwa yapo chini ya wananachi ambao walikuwa wakiyatumia kuvuna na kuuza mchanga huo kwa wamiliki wa magari na kampuni mbalimbali za ujenzi. Mwakilishi wa Mfenesini, Machano Othman Said alisema  pamoja na rasilimali hiyo kuonekana kupungua kwa kiwango kikubwa, haikusatahili wananchi kupokonywa mashamba yao bila makubaliano maalumu. Mwakilishi wa Kijitoupele, Ali Suleima Ali ‘Shihata’ alisema utaratibu uliowekwa na Se...

Mtoto Akatwa Makalio na Baba ake

Image
Mwanamume mmoja mkazi wa Ndofe wilayani Nyamagana mkoani Mwanza amemfanyia kitendo cha ukatili mtoto wake kwa kumkata na kisu sehemu za makalio kwa madai ya utoro shuleni. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Nuhu James (50) anayedaiwa kumfanyia ukatili mtoto Ndalo Nuhu (14) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya Sekondari Igoma kwa kumfunga kamba miguuni na mikononi kisha kumchapa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baadaye kumkata na kisu sehemu za makalio, tukio analodaiwa kulifanya majira ya saa 11:00 alfajiri ya tarehe 25 Mei, 2017. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa aliaamua kumfanyia ukatili wa aina hiyo mtoto wake baada ya kugundua kwamba mwanaye ni mtoro shuleni. Kamanda Msangi amesema baada ya mama wa mtoto alipoona ukatili anaofanyiwa mwanaye na hali yake kiafya kuzidi kubadilika alishindwa kuvumilia na jana (Tarehe 28 Mei.2017) aliamua kutoa taarifa kituo cha polisi Kamanda Msangi ameendelea kusema kuwa polisi wapo katika upe...

Mapya Yaibuka: Maafisa wa TMAA Walihongwa Mabilioni ya Pesa Ili Smelter ya Kuchanjua Mchanga wa Madini Isijengewe Tanzania..!!!

Image
Kuna mambo mapya yanayozidi kujitokeza tangu rais Magufuli awasimamishe maafisa wakuu wa Taasisi ya TMAA inayosimamia MADINI ambayo pia ilimfanya rais Magufuli kumvua Uwaziri Mh.Muhongo kama Waziri wa Madini kwa sababu zilizo wazi. Inavyosemekana ni kuwa mwaka wa 2009 TUME maalumu iliyojulikana kama PRESIDENTIAL MINING REVIEW COMMISSION,iliyoongozwa na JAJI Mark Bomani. Tume hii ilitoa MAPENDEKEZO kuwa SMELTER ijengwe hapa nchini. Lakini cha kushangaza ni kuwa maafisa hao wa TMAA wakawa tayari wamekuwa COMPROMISED na Makampuni husika yaani WAKAHONGWA ili WANAYAMAZISHE matakwa ya Tanzania Kuwa na UWEZO wake na TEKNLOJIA HIYO. Katika mbinu zao za kuzima ripoti na mapendekezo ya tume TMAA, miaka sita iliyopita hivi wakaanza mipango ya KUYAMWAGIA MAJI mapendekezo YOTE ya Tume ya Jaji Mark Bomani ili KUIDHOOFISHA kabisa Na mwishowe KUZIZIMA kabisa NDOTO za Watanzania kuwa na mitambo yao ya SMELTER. Na hivyo KUTUSALITI sawasawa ili tuendelee KUIBIWA VIZURI na hayo Makampuni. Mwaka wa 2011 MA...

Ikulu ya JPM Yafafunguka Haya Kuhusu Malalamiko ya Kampuni ya Acacia Juu ya Ripoti ya Mchanga wa Madini..!!!

Image
Uamuzi wa Serikali kuhusu suala la usafirishaji wa mchanga wa madini, utategemea ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza suala hilo. Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Gerson Msigwa ikiwa ni siku moja baada ya kampuni ya Acacia kuitaka Serikali kuunda kamati huru kuchunguza kiasi cha madini kwenye makontena yake 277 yaliyozuiwa bandarini. Wiki iliyopita, Rais Magufuli alikabidhiwa ripoti na kamati ya kwanza iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ambayo ilibaini kuwa makontena hayo yana tani 7.8 za dhahabu. Pia, Acacia wanadai hawakupewa ripoti ya kamati hiyo licha ya kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi. “Sijui chochote kuhusu hao Acacia kuomba iundwe kamati huru, lakini tunasubiri ripoti ya kamati ya pili iliyoundwa kuchunguza sakata hili wampelekee ripoti Rais,” alisema Msigwa. Wakati Ikulu ikisema hayo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alizungumzia ripoti ya kamati ya Profesa Mruma na kusema chanzo cha hayo ni sh...

Hivi Ndivyo Madini Aliyoshtukia JPM Yanavyosakwa Duniani...!!!

Image
WAKATI Rais John Magufuli akikazia msimamo wa kuzuia usafirishaji nje ya nchi makontena ya mchanga wa dhahabu (makinikia), imebainika kuwa baadhi ya madini yaliyotajwa kuwamo katika mchanga huo, yanasakwa kwa udi na uvumba kutokana na umuhimu wake kiuchumi. Aidha, imebainika kuwa mataifa yaliyopiga hatua kubwa kiuchumi kwa kuzalisha bidhaa za kielektroniki kama China na Japan, hutegemea madini hayo katika uzalishaji wa bidhaa kama simu za mkononi, kompyuta, DVD, vifaa vya ndege, betri za magari, satelaiti na hadi utengenezaji wa vinu vya nyuklia. Jumatano iliyopita, Rais Magufuli alipokea ripoti kutoka kwa kamati teule aliyoiunda kuchunguza kila kilichomo katika makontena 277 yaliyoshikiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam ili mwishowe kulinda mapato ya nchi. Matokeo ya ripoti hiyo, iliyowasilishwa na mwenyekiti wake, Prof. Abdulkarim Mruma, yalionyesha kuwa kwa ujumla, thamani ya madini yote yaliyokutwa ni Sh. bilioni 829.4 kwa kutumia viwango vya wastani na Sh. trilioni 1.44 kwa kutu...

BAADA ya Kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki..Museveni Ajipa Ziara za Ulaya..!!

Image
                            Mkataba wa Ushirikiano wa Kibiashara (EPA) baina ya nchi wanachama wa Jumuiya ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Nchi za Umoja wa Ulaya (EU), bado halijapatiwa ufumbuzi mpaka hivi sasa. Baada ya Tanzania na Uganda kugoma kusaini mkataba huo wa ushirikiano ambao baadhi ya viongozi wanaufananisha na ukoloni mambo leo, viongozi hao wamekubaliana kutuma ujumbe mjini Brussels, Ubelgiji yaliko makao makuu ya EU ili kujadili kwa kina juu ya EPA na kufikia ufumbuzi. Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo ambaye pia ni Rais wa Uganda, Yoweri Museveni atakwenda huko ili kujadili nafasi ya kiuchumi ya EAC na pia kuzungumzia suala la kutoiadhibu Kenya kutokana na nchi wanachama kutosaini mkataba huo. Akizungumza katika mkutano wa 18 wa wakuu wa nchi za EAC mara baada ya kukabidhiwa kijiti cha kuiongoza jumuiya hiyo na Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Rais Museveni alisema...

Wakandarasi waanikeni wanao waomba Rushwa

Image
                                 SERIKALI imewataka wakandarasi nchini kuwafichua maofisa wa serikali ambao wamekuwa wakiwaomba rushwa ili wawapatie zabuni za ujenzi wa miradi. Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Joseph Nyamhanga, wakati akifunga Mkutano wa Mwaka wa Mashauriano kwa Wakandarasi mjini Dodoma. Mkutano huo uliofunguliwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, uliandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wakandarasi (CRB), na ni wa kila mwaka ambapo wakandarasi hukutana na kuzungumzia changamoto zinazowahusu na kuziwasilisha serikalini. Nyamhanga alisema kuna umuhimu mkubwa wa kushirikiana kupambana na rushwa kwenye utoaji wa zabuni kwani imekuwa ikisababisha miradi kuchelewa ama kutekelezwa kwa kiwango cha chini. “Kwenye hili naomba muipe ushirikiano mkubwa CRB na serikali tuwabaini hawa watu maana wanakwamisha ustawi wa miundombinu yetu, wata...