Posts

Showing posts with the label SIASA

Kimenuka..Ofisi ya CCM Yachomwa Moto Pwani

Image
Watu wasiojulikana wameichoma moto ofisi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) tawi la Mshonzini iliyopo Wilayani Mafia Mkoani Pwani na kuteketeza mali mbalimbali za chama hicho. Katibu wa CCM Wilayani Mafia, Mohammed Dhikiri, amethibitisha kutokea kwa tukio na kusema ofisi hiyo imechomwa moto usiku wa kuamkia leo na kuongeza kuwa moto huo umeteketeza kabisa ofisi hiyo na samani za ndani. Bw. Mohammed amesema bado haijajulikana sababu za ofisi hiyo kuchomwa moto kwa kuwa wakati tukio linatokea hakukuwepo na viashiria vyovyote vya vurugu miongoni mwa wanachama wa chama hicho. Naye Mbunge wa Mafia, Mbaraka Dan, amesema, vipo viashiria vinavyoonesha kuwa alifika mtu asiyejulikana karibu na ofisi hiyo kisha kuwasha na kurusha kijinga cha moto kwenye paa la makuti la ofisi hiyo na kwamba, mtu huyo baada kutekeleza kitendo hicho aliondoka kuelekea kichakanani kama ambavyo alama za nyayo za miguu yake zinavyoonesha.

TAARIFA ya CHADEMA Kuhusu Lowassa Kuitwa Polisi

Image
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Edward Lowassa amepata wito kutoka kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kumtaka kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi kesho Jumanne, saa 4 asubuhi kwa ajili ya mahojiano. Mhe. Lowassa ambaye pia alikuwa Mgombea Urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia CHADEMA, kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita, hajapewa maelezo wala ufafanuzi wowote kuwa mahojiano hayo yatahusu nini hasa. Tayari Chama kimetoa maelekezo kwa Kurugenzi ya Katiba na Sheria ya Chama kuhakikisha kuwa Mhe. Lowassa anapata msaada wa kisheria wakati wa mahojiano hayo. Taarifa za awali zinaonesha kuwa mahojiano hayo yanahusishwa na kauli za Mhe. Lowassa alizotoa katika nyakati tofauti hivi karibuni wakati akishiriki futari pamoja na Watanzania wenzetu Waislam waliokuwa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, ambapo amekuwa kiitaka Serikali kuzingatia misingi ya utawala bora kama mojawapo ya misingi muhimu ya kuendesha nchi kwa a...

CHADEMA Watoa Ushauri kwa Rais Magufuli Sakata la Madini......Wasema Wapo Tayari Kushirikiana Nae

Image
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimedai kuwa kipo tayari kumuongoza Rais John Magufuli katika kulinda rasilimali za Taifa ikiwemo madini, huku kikiwataka wananchi kuishauri serikali kuchukua hatua kwanza badala ya kuipongeza kuhusu sakata la Makinikia. Wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Chadema, Dkt. Vincent Mashinji amedai kuwa, hatua anazochukua Rais Magufuli kuhusu Makinikia ziko kinyume na Ilani ya CCM ambapo katika ukurasa wake wa 26-28 haikuzungumzia kurekebisha sheria na mikataba ya madini, na kwamba ilani ya Chadema kwenye ukurasa wake wa 57-59 inaonyesha namna ya kuiongoza vizuri sekta ya madini. “Rais hatafaulu vita hii kama serikali yake itaendelea kutubagua au kutosikiliza sauti ya upande wa pili. Pia watu wasiwe wa kutoa pongezi kabla kazi haijaisha. Kama tunatakiwa kulipwa trilioni mia, wajue kwamba za kwetu ni asilimia 4 tu, na hii ndiyo matokeo ya mikataba tuliyoilaani kila siku. mrabaha wetu ni asilimia 4 huku wa...

JPM Avionya Vyombo vya Habari Vinavyowataja Kikwete, Mkapa Sakata la Makinikia

Image
Rais John Magufuli amevionya vyombo vya habari vinavyowataja marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wakiwahusisha na sakata la mchanga wa madini.  Rais Magufuli ameyasema hayo leo (Jumatano) Ikulu baada ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya nchini Canada, Profesa John Thornton. Barrick Gold Corporation ni kampuni mama ya kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia. “Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike,” amesema  Rais. Ameonya viongozi hao kuhusishwa katika taarifa za kamati mbili za uchunguzi wa madini yaliyo katika makontena yenye mchanga wa madini (makinikia).

Live Updates:Haya Hapa Ndio Mambo Yaliyogunduliwa na Kamati ya Wanasheria na Wachumi ya Kuchunguza mchanga wa Madini

Image
1.Kamati ya wanasheria na wachumi ya kuchunguza mchanga wa madini iliteuliwa Aprili 10 ikiongozwa na Prof. Nehemiah Osoro. 2.Miongoni mwa hadidu za rejea ambazo kamati ilipewa ni kujua idadi ya makotena yaliyosafirishwa nje ya nchi tangu 1998. 3.Kamati pia ilitakiwa kuchunguza kama Tanzania inauwezo wa kutengeneza 'smelter' nchini, gharama zake na muda utakaotumika. 4.Kamati ilitakiwa kuchunguza tofauti ya mapato ambayo Tanzania ilipata na ambayo ilitakiwa kuyapata tangu mwaka 1998. 5.ACACIA inayojinasibu kama mmiliki wa migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi haijawahi kuwasilisha nyaraka za umiliki huo. 6. Kamati imebani kwa mujibu wa nyaraka kuwa kampuni ya ACACIA PLC haikusajiliwa nchini 7.Kamati imebaini kuwa wamiliki wa makampuni ya madini nchini wametenda makosa mbalimbali ya jinai. 8.Kamati imeridhia baadhi ya watumishi wa serikali, makampuni ya usafirishaji na TMAA wameliingiza Taifa hasara kwa makusud. 9.Makampuni ya Pangea na Bulyahulu yamepatikana na hatia ya kuliingizia Ta...

Sumaye Nchi Inaendeshwa Kishabiki

Image
                                      WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Fredrick Sumaye, amesema nchi inashindwa kuendelea kwa sababu inaendeshwa kishabiki  na kwamba mambo yanayofanyika hayana masirahi kwa taifa. FREDRICK SUMAYE. Akizungumza kwenye  Kongamano la Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) na Umoja wa Vijana wa Vyuo Vikuu ambao ni wanachama wa Chadema (Chaso) jijini Mbeya alipokuwa mgeni rasmi, Sumaye alisema mambo mengi yenye masirahi ya taifa yakifanywa kimzaha yatasababisha madhara kwa taifa. Sumaye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, alisema miongoni mwa mambo ambayo ni ya maslahi ya taifa lakini  yanendeshwa kishabiki ni mikataba ya madini na bajeti isiyokuwa na uhalisia. Mengine aliyoyataja ni uendeshaji wa Bunge ambalo kikatiba ni chombo huru ambacho hakipaswi kuiingiliwa n...

Maalim Seif Alaani Adhabu ya Mdee, Bulaya..!!!

Image
                                 Siku chache baada ya Bunge kuwazuia wabunge Halima Mdee na Ester Bulaya kuingia vikao vyote vya Bunge hadi Bunge la Bajeti mwakani, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema vitendo hivyo ni mwendelezo wa kupigwa mateke kwa demokrasia Tanzania. Pia amesema hiyo ni ishara kuwa watawala waliopewa madaraka hawataki kufuata misingi ya demokrasia iliyopo. Mdee na Bulaya wote kutoka Chadema walikumbana na adhabu hiyo kutokana na vitendo vyao wakati Spika Job Ndugai alipoagiza Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ambaye alipewa adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge hili linaloendelea, aondolewe ukumbini wakati wa mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini. Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe, alionekana akimvuta shati mmoja wa askari waliokuwa wakimtoa Mnyika, wakati Bulaya wa Bunda Mjini alionekana akiwashawishi wabunge wa upinzani kutoka nje kuonyesha mshikamano kupinga ua...

Zitto: Tumemtoa Mghwira Ili Kuondoa Dhana Kwamba ACT ni "CCM B"..!!!!!

Image
  Mbunge wa Kigoma Mh Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa ACT wazalendo amesema kwamba wameamua kumuweka pembeni mwenyekiti wao wa zamani Mama Anna Mghirwa ili kutoa dhana kwamba ACT ni CCM B. "Sasa tunaweka kanuni ambazo mtu akichaguliwa na uongozi wa juu unaoongozwa na Chama kingine tofauti na ACT basi tufanye kwanza mazungumzo kabla ya mtu kukubali tu bila kutoa taarifa" alisema Mh Zitto Kabwe. Pia akaongeza kwa kusema kwamba kwa sasa wameshachagua kaimu mwenyekiti wao wa Chama na anaendelea na majukumu kama kawaida.

Ukweli Mchungu..Rufaa ya Kambi Rasmi ya Upinzani Dhidi ya Adhabu ya Mdee na Bulaya ni Hopeless na ni Kupoteza Muda Tu..!!!

Image
Kuna taarifa kuwa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wamekata rufaa kupinga adhabu waliyopewa Wabunge Halima Mdee na Ester Bulaya (CHADEMA). Wabunge hao wamefungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa kipindi cha miezi kumi. Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, Toleo la 2013, Wabunge hao watapokea nusu mshahara na nusu posho kwa kipindi chote cha adhabu yao. Rufaa hiyo, kama ipo kweli, ni hopeless, kupoteza muda na haitafanikiwa. Kuna sababu mbili za kisheria na kiuhalisia. Kwanza, Kanuni za Bunge hazina neno 'rufaa' au 'rufani'. Yaani, hakuna suala la rufaa kwa jambo lolote linaloamuliwa na Bunge (niko tayari kurekebishwa). Katika adhabu zinazotolewa na Bunge, kwa mujibu wa Kanuni ya 74 ya Kanuni za Bunge, hakuna rufaa inayozungumziwa. Kukosekana kwa kifungu maalum katika Kanuni za Bunge kinachohusu rufaa dhidi ya adhabu kwa Wabunge ni pengo kubwa kisheria katika kuwasilishwa, kusikilizwa na kuamuliwa kwa rufaa hiyo inayosemwa kuwasilishwa. Bunge, au Mamlaka iliyopelekewa rufaa, hal...

Hatma ya Mhe Anna Mghwira Kuendelea na Uenyekiti wa ACT Wazalendo Kujulikana Leo..ACT Wakutana Kumjadili..!!!

Image
                                                 Wakati Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amekula kiapo Ikulu jijini hapa jana, Jumanne Chama cha ACT- Wazalendo kimesema kitajadili utekelezaji wa majukumu yake mapya na ya uenyekiti wa chama hicho. ACT imesema ilipokea taarifa ya uteuzi huo wakati Mghwira akiwa nje ya nchi hivyo baada ya kurejea, viongozi wa juu wa chama hicho pamoja na yeye walifanya mazungumzo kuhusu uteuzi huo. Mghwira aliteuliwa nafasi hiyo Juni 3, mwaka huu na Rais John Magufuli kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Saidi Meck Sadick aliyeamua kuachia ngazi ili vijana waendelee kufanya kazi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana Jumanne na kuthibitishwa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa ACT, Ado Shaibu ni kuwa kufuatia uteuzi huo na uenyekiti na majukumu ya Mkuu wa Mkoa kamati ya uongozi wa chama...

Waziri Mkuu Awatuliza Wabunge Sakata la Madini ya Mchanga ( Makinikia)

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wawekezaji wa madini nchini kuondoa hofu ya kukosa haki zao kwani kamati ya pili iliyoagizwa kufanya uchunguzi kuhusu mchanga wa madini (makinikia) bado haijakamilisha kazi yake.  Waziri Mkuu alisema hayo jana wakati akijibu swali la mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka, lililohoji kuhusu taswira ya Tanzania kimataifa hasa katika uwekezaji wa madini. Majaliwa aliwataka wawekezaji wa madini kuondoa hofu kwa kuwa  kamati ya pili iliyoundwa kuangalia athari za kisheria, kisiasa na kimataifa kuhusu sakata la mchanga wa madini bado haijatoa ripoti yake. “Watanzania wengi walikuwa na hofu, hata wabunge wengi katika serikali hii ya awamu ya tano mmekuwa mkizungumzia sakata la mchanga wa madini, lakini niwatoe hofu,  Rais John Magufuli alifanya hayo kwa nia njema ya kulinda rasilimali za Taifa,” amliema Waziri Mkuu aliwataka wawekezaji wa madini kuondoa hofu kwa kuwa  serikali itazingatia ushauri kutoka sekta nyingine kabla ya kuc...

Lissu; Nia Njema ya Magufuli Inatupeleka Pabaya..!!!!

Image
                          Suala sio nia njema ya Rais. Suala ni consequences za hiyo nia njema. The road to hell is paved with good intentions. Mugabe most likely alikuwa na nia njema. The consequences za nia njema hiyo ni kwamba Zimbabwe ya leo haina hata sarafu yake na imegeuka kuwa ya kuomba chakula wakati ilikuwa a major food exporter. Kama kweli Rais Magufuli ana nia njema angeanza na mfumo mzima wa kisheria, sio kuhangaika na magwangala. 100% ya uzalishaji wa dhahabu ya Geita unafanyikia mgodini na Geita Gold Mine ni mgodi mkubwa kuliko yote nchini. Kwa logic ya Magufuli ni kwamba GGM hawatuiibii kwa sababu tu smelting yote inafanyikia Geita. Acacia wanayeyushia dhahabu yote ya Nyamongo mgodini Nyamongo. Kwa logic hiyo hiyo, hawa wezi wa mchanga wa Bulyanhulu na Buzwagi hawaibi Nyamongo kwa sababu tu wanafanya kila kitu Nyamongo. Resolute walisafisha 100% ya dhahabu yao Nzega mpaka walipokomba kila kitu na kuacha ma...

Polepole aonywa kauli yake ya Mauaji Kibiti

Image
Mwenyekiti wa Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemuonya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hampyrey Polepole aache mara moja kugeuza matukio ya kuuawa Watanzania  katika Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani kwa kuyageuza kama mtaji wa kisiasa kwa CCM ili CCM ionewe huruma na kuvichonganisha vyama vingine na wananchi. Mgeja alisema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari akiwa mkoani Morogoro akitokea Dar-s-Salaam. Mgeja alisema kila mpenda amani nchini amesikitishwa na kauli yenye ukakasi alizotoa Polepole hivi karibuni akisema CCM inakemea na imekuwa ikikemea maafa hayo lakini vyama vya upinzani vikikaa kimya. Mwenyekiti huyo amemshangaa Polepole kwa maneno yake akimtaka atambue kila Mtanzania mpenda amani kwa matukio yanayotokea wilayani Mkuranga, Kibiti na Rufiji mkoani Pwani yanawagusa moja kwa moja bila kujali dini zao, ukabila wao wala vyama vyao vya siasa. “Tumesikitishwa kwa kauli za Polepole za kwake bila kujali msingi na wala siyo kipindi muafaka wakati taifa ...

Mbowe: Tunajiandaa Kukamata Dola Mwaka 2020...!!!

Image
                               Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema wamebadili msingi wa uongozi wao ikiwamo kufanya mfumo unaoendana na mwaka wa Serikali ambao unaanzia Julai Mosi hadi Juni 30. Kwa mujibu wa Mbowe, Chadema imefanya hivyo kutokana na maandalizi yao ya kushika dola mwaka 2020 na kuwa ndiyo maana wameanza kufanya hivyo mapema. Akifungua mkutano wa Baraza Kuu mjini Dodoma jana, Mbowe aliwataka wajumbe na wanachama kukubaliana na mabadiliko hayo kutokana na hali ilivyo kwa sasa baada ya kuona chama kinakwenda vizuri na kinazidi kukua kila kukicha. “Nasisitiza kuwa, lazima chama hiki tukilinde na kukijenga kwa gharama zote, tumepita milima na mabonde lakini ukweli hata ninyi mnajua kuwa tuko mahali salama sasa,” alisisitiza. Awali, Katibu Mkuu wa Chadema Dk Vicent Mashinji alisema chama kinakua kwa kasi ya ajabu ambayo wengi wanashindwa kuijua. Alisema kwamba mpango walionao ni kuhakikish...

UKWELI Mchungu..Ulipumba Unadumaza Demokrasia Nchini...!!!!

Image
                                  KATIKA siasa za Tanzania kuna kupakaziana kwa kila aina, walio madarakani huwakazia wa upande ule wanaoitwa wapinzani. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kiliitwa chama cha Wachaga kwa sababu mwaasisi wake ni Eddwin Mtei. Hawakusema lolote kwa aliyekuwa Makamu wake, Bob Makani (marehemu) ambaye ni Msukuma wa Shinyanga. Baadaye siku zilivyokuwa zinasogea na Chadema kushika moto Kanda ya Kaskazini, wa upande wa pili wakasema chama cha ukanda kupitia Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, Mwenyekiti Freeman Mbowe. Ujio wa waliokuwa mawaziri wakuu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, ukatafsiriwa, wakipewa nchi ni hatari na kwamba wataigawa nchi kikanda. Nadhani ni kutokana na mtazamo huo, Freeman Mbowe akamteua Dk. Mashinji Msukuma kutoka Kanda ya Ziwa, ili kuifuta ile dhana ya Chadema kuwa chama cha Ukanda wa Kaskazini. Kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF), wa upande...

Askofu Gwajima awajia juu wanaoizungumzia nchi vibaya

Image
                             Dar es Salaam.Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewaonya baadhi ya watu wanaoiongelea vibaya nchi akiwataka waache mara moja kwa kuwa wanachochea uvunjifu wa amani. Askofu Gwajima amesema kinachotakiwa watu waizungumzie nchi vizuri kwa kuwa amani itakuwepo na uchumi wa nchi utaendelea kukua. "Namkemea yule mtu ambaye anaiongelea vibaya nchi yetu huwezi ukawa unatoa kinywa kinachoashiria uvunjifu wa amani," "Huwezi kila siku unalaani kwa kuiongelea vibaya nchi yetu lazima nikemee ili nchi yetu iweze kuendelea kuwa na amani,"amesema Gwajima katika mahibiri kanisani kwake leo.

Mbowe Azua Jipya..Adai Bajeti ya Serikali Haitekeleziki..Wajiandaa Kuipinga Bungeni

Image
                                       Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema wataipinga bungeni bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2017/18 kwani haina msaada wowote kwa wananchi wa hali ya chini na wanaamini fedha hizo hazitapatikana kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo. Mbowe amesisitiza mwaka jana wabunge wa kambi ya upinzani walieleza wazi kuwa bajeti ya mwaka huu isingetekelezeka na ndio kilichotokea kwani mpaka sasa asilimia 34 pekee ya pesa zote za maendeleo ndizo zimetolewa.

Huu Ndio Ujumbe wa Mbunge Husein Bashe wa CCM,Ambao Umekuwa Gumzo Mitandaoni

Image
                            Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe (CCM)amechapisha ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram wenye maneno haya. “Kama taifa wazee wetu walipoanzisha harakati za kudai uhuru na hatimaye tukaupata mwaka 1961 walikuwa na malengo‘ “Upo uwezekano mkubwa kwamba sisi viongozi wa sasa tumewaangusha ninyi raia katika kufikia malengo ya waasisi wetu ‘Msikubali kuangushwa na sisi wachache, nyinyi ni wengi mna mamlaka na nguvu ya kututaka sisi kuwafikisha kwenye malengo ya Uhuru‘ –Hussein Bashe ‘Ni jambo la hatari kwa taifa inapotokea viongozi wakakosea na kutoka nje ya malengo, wananchi wakakaa kimya na kuogopa kuonya, kushauri, kukosoa au hata kukemea sababu tu ya woga au hofu. ‘Tutakua tunajenga taifa la raia waoga msiingiwe na woga juu ya kudai haki zenu na kututaka sisi viongozi kutimiza wajibu wetu ‘Kwa kushindwa kwenu kutukemea au kutushauri tunapokengeuka sote tunaingia katika kundi moja la k...