Warioba Apigilia Msumari Baa la Njaa Nchini...

                
Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Sinde Warioba amesema haina haja ya kubishana kama kuna njaa au upungufu wa chakula kwani dalili zinaonyesha tatizo hilo litatupata na haitakuwa mara ya kwanza kwani limeshawahi kutokea.

Amesema kuwa wakati wa nyuma tatizo kama hilo lilipotokea watu walishirikiana kusaidia kuwapa wakulima maarifa na taarifa za hali ya hewa ili waweze kukabiliana na tatizo.

Ametolea mfano njaa inavyoathiri nchi za Somalia, Kenya na Nigeria kwa sasa ambapo watu na mifugo wamefariki na kusema mabishano hayasaidii.


Ameyasema hayo yote katika Kongamano la wanawake katika Uongozi linaloendelea katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Hatma ya Mhe Anna Mghwira Kuendelea na Uenyekiti wa ACT Wazalendo Kujulikana Leo..ACT Wakutana Kumjadili..!!!

Matamshi ya Magufuli kuhusu wasichana wa shule waliotungwa mimba yawakasirisha wanawake Tanzania

Kinana Amjibu Kikwete Juu ya Mabadiliko ya CCM..!!!