Dc Chongolo Ataka Serikali Isipeleke Chakula Cha Njaa

Wananchi wa jamii ya kifugaji hususani vijijini wametakiwa kuacha kulalamika kuna njaa na badala yake watumie mifugo wanayofuga kuuza katika minada na kisha kununua chakula cha kutosha majumbani mwao na kuondoa tafsiri ya kupatiwa chakula na Serikali ili hali wanamifugo.
Pia ameitaka Serikali kutowaletea chakula cha njaa,ambapo jamii kubwa imejijengea tabia ya ya kutoacha chakula cha ziada kwa ajili ya Serikali badala yake kutegem,ea kuwa Serikali ittawaletea chakula cha msaada badala yake wabadili mtazamo na tabia zao za kuweza ziada na kuhifadhi chakula endepo kutakuwa na uhaba wa chakula kam hivi sasa kumekuwa na uhaba wa mvua hali ambayo mazao yamekuwa hayastawi kama awali.
Hata hivyo katika hoja hizo Mkuu wa wilaya ya Longido Daniel Chongolo akatumia nafasi hii kuwataka viongozi wasiwajengee wananchi kuwa kuna njaa na badala yake wawajengee uwezo pindi wanapouza mifugo yao wasitumie fedha zao katika masuala mengine na badala yake wanu nue chakula na kwamba yeye katika wilaya yake haitaji msaada wa chakula kwani wananchi wake si masikini wa kununua chakula.
Mkoa wa Arusha umejaaliwa kuwa na wilaya Zaidi ya sita ambapo wananchi wengi wa vijijini ni wa jamii ya kifugaji ambapo katika kipindi cha hivi karibuni kulizuka mjadala kuwa maeneo ya wilaya za Mkoa huo kuna njaa ambapo serikali imekuwa ikipingana vikali na kauli hizo za wananchi na kuzua mjadala mkubwa kwa wananchi.
Comments
Post a Comment