Posts

Showing posts from December, 2016

WASHITAKIWA Wanne Mauaji wa Dr. Mvungi Waachiwa Huru

Image
  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru washitakiwa wanne kati ya 10 waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya mauaji ya bila  kukusudia ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi. Washitakiwa walioachiwa ni Masunga Makenza (40), mkazi wa Tabata Darajani, Zacharia Msese (33), Ahmad Kitabu (30) mkazi wa Mwananyamala na John Mayunga (56). Waliachiwa kwa mujibu wa Kifungu Namba 91 Kifungu kidogo cha kwanza cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA). Wakili wa Serikali, Pamela Shinyambala alidai mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba kuwa upande wa mashitaka umeshasajili jalada hilo Mahakama Kuu. Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mshitaka Nchini (DPP), hakuwa na nia ya kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao kwa mujibu wa kifungu hicho. Awali, Shinyambala alidai kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutolewa maelezo ya mashahidi baada ya upelelezi wa kesi hiyo kukamilika. Hakimu Simba alisema anawaachia washitakiwa hao, kama walivyoomba upande wa mashitaka. Alisema ...

HOJA Sita za rufaa ya Mbunge Lema Kusikilizwa leo

Image
  Hoja sita za mawakili wa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema kupinga kunyimwa dhamana zinatarajiwa kusikilizwa leo mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu, Salma Maghimbi.  Wakili Sheck Mfinanga anayemwakilisha Lema alisema waliwasilisha hoja hizo za rufaa kupinga uamuzi wa kunyimwa dhamana mteja wao.  Lema aliyekamatwa Novemba 2, akiwa mjini Dodoma, tangu wakati huo anashikiliwa kwenye Gereza Kuu la Kisongo jijini Arusha ambako amekaa kwa siku 56.  Baada ya kukamatwa na kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Lema alipewa dhamana na Hakimu Mkazi Desdery Kamugisha katika kesi namba 440 na 441/2016 akidaiwa kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli.  Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) alikata rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama kumpa dhamana mbunge huyo. Mawakali wa Lema nao walikata rufaa kupinga mteja wao kunyimwa dhamana ambayo imepangwa kusikilizwa leo baada ya kukwama kwa muda mrefu kutokana na kuwapo pingamizi za kisheria zilizowasilis...

TUNDU Lissu Akamatwa na Jeshi la Polisi

Image
  TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam “Nashikiliwa na polisi hapa Kituo Kikuu kutokana na ile press conference (mkutano na waandishi wa habari) kuhusu kupotea kwa Ben Saanane,” alimweleza mwandishi wa habari hii kupitia simu leo. Mwandishi alimtafuta Lissu kutaka kujua baadhi ya mambo, ndipo alipopokea simu na kueleza hivyo. Hakuna taarifa zaidi mpaka sasa. Saanane ambaye ni Msaidizi wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa-Freeman Mbowe alipotea ghafla takribani mwezi mmoja sasa na hajulikani alipo. Wafuasi wa CHADEMA wamekuwa wakimsaka kiongozi huyo bila mafanikio yoyote jambo ambalo limeendelea kuzua hofu kama yu hai ama ameuawa. Tarehe 14 Desemba mwaka huu, Lissu alizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam akiomba vyombo vya ulinzi kusaidia kupatikana kwa kiongozi huyo. Chanzo: Mwan...

Polisi Waua Wawili kwa Tuhuma za Ujambazi

Image
  Polisi wilayani Rungwe wamewaua watu wawili kwa tuhuma za ujambazi baada ya kuanza kufyatua risasi kwa polisi waliokuwa wakiwafuatilia. Kamanda wa polisi mkoani hapa Dhahiri Kidavashari amesema leo kuwa  tukio hilo limetokea  katika Tarafa ya Pakati wilayani humo baada ya polisi kuwafuatilia watu waliokuwa na nia ya kwenda kufanya ujambazi  katika duka la mfanyabiashara wa soda na bia za jumla na M-Pesa katika Kijiji cha Kisiba. Alisema  majambazi watatu walipakizana kwenye pikipiki moja na baada ya kuwaona polisi walianza kufyatua risasi na hatimaye polisi walijibu na kuwajeruhi wawili kati ya watatu huku mmoja akifanikiwa kutimua mbio baada ya kuitupa bunduki.

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa Apokea Msaada Wa Maafa Ya Tetemeko La Ardhi Kagera

Image
  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea fedha taslimu sh. milioni 10 kutoka Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) zikiwa ni msaada kwa ajili ya watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano ya mchango huo yamefanyika leo mchana (Alhamisi, Oktoba 22, 2016) kwenye Makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Akikabidhi mchango huo, Askofu Mkuu wa Kanisa la EAGT, Dk. Brown Mwakipesile amesema kanisa hilo limeona lina wajibu wa kuisadia Serikali kuwapunguzia machungu watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17. “Tumeona ni vema kanisa la EAGT lishiriki kuisadia Serikali kuwafariji wananchi waliopata maafa kutokana na tetemeko hilo. Tumeona ni wajibu wetu kwa sababu waliopatwa na maafa ni watu wetu wote. Tunawaombea wote waliopatwa na shida waweze kupata nafuu mapema zaidi,” amesema. Askofu Mkuu Dk. Brown ametumia fursa...

RC: Machinga Lazima Waondoke

Image
  JOHN Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amesema kuwa, mpango wa kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) katikati ya Jiji la Mwanza upo pale pale, anaandika Moses Mseti. Tarehe 3 Desemba, mwaka huu wakuu wa wilaya mbili za Nyamana na Ilemela, walianza kutelekeza agizo la Mongella la kuwaondoa machinga kutoka katikati ya jiji kabla ya Rais John Magufuli kuagiza kuchwa waendelee na shughuli zao kama kawaida. Mongella ametoa kauli hiyo leo wakati wa kikao cha pili cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mwanza (RRB) kilichofanyika katika ofisi za mkuu wa mkoa huo. Kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika tarehe 28 Julai mwaka huu kilizungumzia suala la machinga kuondolewa katikati ya jiji lakini washiriki wa kikao hicho waliazimia wafanyabiashara hao watengewe maeneo ambayo ni rafiki kwa shughuli zao. Mongella amesema kuwa, zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara hao lililositishwa na rais Magufuli tarehe 6 Desemba mwaka huu, limetafsiriwa vibaya na Wananchi kwamba, machinga wana...

Polepole atangaza 'vua gamba' ya CCM kivingine

Image
Mabadiliko yaliyofanywa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yamekuja na mkakati mpya wa kuwavua ‘gamba’ makada wa chama hicho wenye ukwasi waliovuna kinyume na taratibu. Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole amesema kuwa wako katika mkakati wa kukisafisha zaidi chama hicho, akiwataka matajiri wenye ‘makandokando’ wajiondoe mapema. “Kuwa tajiri si dhambi na si kwamba CCM inafukuza matajiri, hapana. Tatizo letu kama CCM katika mwelekeo mpya, mtazamo mpya na maegeuzi yanayofanyika, hatuhitaji kuwa na aina ya matariji wanaojipatia utajiri wao kwa hila, kwa rushwa na kwa dhuluma,” alisema Polepole katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini. “Ukijiona wewe ni tajiri na mikono yako ni michafu kwa maana ya kuwa na makando ya kukosa uaminifu, hulipi kodi, ukae mbali na CCM,” aliongeza. Alisema watawachukulia hatua za kuwaondoa ndani ya chama hicho na kuwakabidhi kwa vyombo vya dola ili wachukuliwe hatua za kisheria. Tangu alipochag...

Mwakyembe Ampongeza Makonda

Image
  WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kitendo chake cha kuwasaidia wananchi wa mkoa huo kupata huduma za msaada wa kisheria na mpango wa kujenga mahakama 20 mpya. Dk Mwakyembe ametoa pongezi hizo jana alipokutana na Makonda ofisini kwake jijini Dar es Salaam wakati viongozi wa wizara hiyo walipomtembelea kumpongeza na kuunga mkono jitihada zake katika kuhakikisha wananchi wa Dar es Salaam wanapata haki zao kwa wakati. “Mkuu wa Mkoa nimekuja hapa hii leo (juzi) na timu yangu kukupongeza na kukuonesha kwamba tunakuunga mkono na tuko pamoja kuhakikisha upatikanaji haki na huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi vinapatikana kwa wakati,” amesema Dk Mwakyembe. Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome alisema wizara imenufaika na ziara ya Makonda ambayo ilimpatia fursa ya kusikiliza kero, malalamiko mbalimbali kutoka kwa wananchi na kuonesha kuwa wananchi wengi...

Kesi Mauaji ya Watafiti Kutajwa Tena Desemba 29

Image
  KESI ya mauaji ya watafiti wa Kituo cha Utafiti cha Selian Arusha (SARI) inayowakabili wakazi 29 wa kijiji cha Iringa Mvumi Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, inatarajiwa kutajwa tena Desemba 29, mwaka huu kutokana na upelelezi wake kutokamilika. Watu hao wanakabiliwa na mashitaka matatu ya mauaji ya watafiti watatu, Nicas Magazine, Theresia Nguma na Faraji Mafuru huku gari lao lenye namba za usajili STJ 9570 aina ya Toyota Hilux Double Cabin likichomwa moto. Washitakiwa katika kesi hiyo ni Amos Kwanga, Mashaka Nyambi, Victoria Lungwa, Wilson Mabwai, Sarah Chimanga na Daud Mangwata. Wengine ni Peter Fwezi, Adrian Sudai, Charles Lemanya Fredrick Sudai na Tibu Ng’ambi, Bruno Lebedu, Jonas Makwawa,Erasto Masaka, Juma Chitongo, Cesilia Mwalu, Dorca Mbehu, Edna Nuno, Grace Masaulwa na Juma Madeha. Wengine ni Albert Chimanga, Sosteness Mseche, Julius Chimanga, David Chimanga, Lazaro Kwanga, Yoram Samamba, Edward Lungwa na Simon Samamba. Awali ilidaiwa na Mwendesha Mashtaka wa S...

Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti aliyetangaza kuwepo kwa ugonjwa zika nchini

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Dk Mwele Malecela. Taarifa hiyo ya Ikulu haikueleza sababu za kutenguliwa kwa uteuzi huo, lakini ni siku moja tangu Mwele kueleza kuwa ugonjwa wa zika upo nchini. Taarifa iliyotolewa usiku huu na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa inasema uteuzi wa mkurugenzi mpya atakayejaza nafasi hiyo utatangazwa baadaye. Akizungumza na waandishi wa habari juzi Alhamisi, Dk Malecela alisema kati ya watu 533 waliopimwa wakati wa utafiti walioufanya, asilimia 15.6 waligunduliwa kuwa na virusi vya zika. Hata hivyo, siku moja baadaye, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alikanusha uwapo kwa virusi hivyo. “Kama nilivyoeleza Februari, ugonjwa huu haujaingia nchini, napenda kuwatoa hofu wananchi, hivi sasa Tanzania haujathibitishwa kuwapo na ugonjwa wa zika,” alisema Ummy Mwalimu. Wizara hiyo inasema uchunguzi uliofa...

Waziri Mkuu Acharuka, Asema NGO Chonganishi Zitafutwa

Image
  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa miezi sita ya kujitathimini mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi zake wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, kama yanafanya kazi kwa misingi ya sheria na maadili. Baadaye, yatahakikiwa na kama yatabainika yanachochea migogoro, yatafutwa. Pia, Majaliwa amezicharukia NGOs nyingine zinazoitangaza vibaya Tanzania kimataifa kwa kupiga picha za kudhalilisha watoto wakiwa wanatembea kwenye mawe huku wamevaa kandambili kubwa, kuonesha nchi ni masikini. Ametaka NGOs hizo kuondoka nchini, la sivyo serikali itazishughulikia. “Hizi NGOs zingine si muondoke, nendeni kwingine mkafanye kazi. Halafu nyie mnaotuma picha za kudhalilisha watoto wakiwa wamevaa kandambili kubwa, kudai nchi za nje eti Tanzania ni masikini, tutawashughulikia,” alisema Majaliwa alipozungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro jana. Aidha alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) atakuja wilayani hapo kukagua kazi walizozifanya, wanazo...

Kitu Afande Sele kaongea toka ajivua uanachama ACT-Wazalendo….

Image
  Ni msanii mkongwe Afande Sele kutoka Tanzania alitangaza kujivua   uanachama wa ACT Wazalendo.Kilichomfanya Afande Sele a-trend kwenye mitandao ya kijamii Dec 15 2016 ni baada ya kuchukua maamuzi hayo ya kujiondoa ndani ya chama hicho cha ACT- Wazalendo. Baada ya hapo wengi wametoa maoni yao kwenye mitandao ya kijamii kuhusu maamuzi ya Afande Sele na usidhani kwamba Afande Sele   mwenyewe hajayasoma, sasa kupitia kwenye Exclusive na Ayo TV na millardayo.com amesema>>>> Ni kweli Dec 15, 2016 nimetangaza rasmi kujiondoa ACT- Wazalendo yaani kujitoa katika masuala ya siasa na sipo katika chama chochote cha siasa sasa hivi mimi ni mtu huru’     ‘Nimejitoa ACT- Wazalendo kwa makusudi kabisa na hili lilikuwa ni jambo tarajiwa, kitu cha kwanza moja ya matarajio yalikuwa baada ya mimi kuingia ACT nakuwa Mbunge ila sasa sikupata Ubunge na kama ningeupata Ubunge basi nisingejitoa ndani ya chama’